MAELFU YA WATU WAHUDHURIA UZINDUZI WA SHILO TANZANIA




Askofu Maboya kutoka Arusha na Askofu Mrisa Kutoka mwanza wakikata utepe kuhashiria uzinduzi rasmi wa Shilo



 Askofu Maboya, Mchungaji msidizi wa Mlima wa Moto Noah Lukumay na mchungaji kiongozi wa Mlima wa Moto Dk. Getrude Rwakatare wakiliombea taifa.




Mwalimu wa nyimbo za Injili Afrika mashariki bwana John Shabani akiongoza uimbaji wa wimbo maalum wa Shilo



Mheshimiwa Mary Mwanjelwa (Mbunge CCM viti Mbeya), akihusika kikamilifu katika kuliombea taifa







Watumishi mbalimbali wa serikali wakiwemo mawaziri wastaafu wkiwakilishwa na wziri Kihula, wakurugenzi, mameneja, wabunge, waalimu, madaktari, wanasheria, wanajeshi wakiombewa ili kuwawakilisha wafanya kazi wote wa serikali

 Vyombo mbalimbali vya habari navyo vimeshiriki kikamilifu

Mama Getrude Rwakatare akimkabidhi kipaza sauti Askofu Maboya kwa ajili ya Neno na maombezi


Kwa mara ya kwanza kongamano la kimataifa la Shilo limezinduliwa Tanzania, ni ndani ya kanisala Mlima wa Moto linaloongozwa na Dk. Getrude Rwakatare.
Hili ni kongamano la kumaliza mwaka na Mungu na kuanza mwaka na Mungu, ni kuanzia tarehe 8-15/12/2013. Katika uzinduzi huo mambo muhimu yamefanyika ikiwa ni pamoja na kuliombea taifa, kuwaombea viongozi wa Taifa la Tanzania, kuwaombea wafanya kazi wa Tanzania pamoja na watanzania kwa ujumla.
Pia katika kuungana na watu mbalimbali duniani katika kuomboleza kifo cha MzeeNelson Mandela, maombi maalum yamefanyika kwa ajili ya familia yake na nchi ya Afrika ya kusini kwa kuondokewa na Mzee wetu Mandela.
Baadhi ya wanenaji katika kongamano la shilo ni Dk. Gtrude Rwakatare mwenyeji, Askofu Danstan Maboya, Askofu Eugene Mrisa, Fransis Junior, Mch. Noah Lukumay na wengine wengi. Vyombo mbalimbali vya habari pia vimehusika kikamilifu katika uzinduzi huo ulioambatana na maombezi ya taifa




Comments