HIVI NDIVYO KANISA LA MLIMA WA MOTO WAKISHIRIKIANA NA PRAISE POWER WALIVYOTEMBELEA KAMBI YA WAZEE NA KUTOA MISAADA MBALIMBALI
Baadhi ya mali ambazo zimekabidhiwa
kijiji cha wazee, Msimbazi jijini Dar es Salaam.
|
Tukio hili ambalo hakika likanikumbusha
kuwa kila mtu atazeeka (Kwa Neema), basi likanipa faraja nikijitazama miaka 97
ijayo, na kuona kundi la watu wakitia kambi ghafla kwenye makazi yangu kunipa
maneno ya faraja na zawadi mbalimbali, inapendeza.
Tukio hilo limeenda sambamba na mpango
wa kanisa hilo wa kutenga mwezi wa novemba kuwa mwezi wa shukrani kwa Mungu.
Akiongea kwa furaha, mmoja wa Viongozi wa Praise Power, Bwana George Mpella, alisema kuwa msukumo wa kufanya jambo hilo
unatokana na Kanisa la mlima wa moto na kituo chao cha Redio, yaani Faraja ya
Watu , kwa hiyo licha ya kuwashauri watu kiimani zaidi, pia mwisho wa siku ni
muhimu kufanya kitu kama hiki kimwili.
Kuna kinamama wana matatizo ya fistula, wakatengwa na jamii na kuna watoto wana matatizo ya kuwa na vichwa vikubwa - hawa wote wamekuwa wakipata misaada kwa namna mbalimbali, lakini ukiangalia wazee - hili ni kundi la watu waliosahaulika, ndio maana Praise Power Radio - Faraja ya Watu na kanisa la Mlima wa Moto tukafanya jambo hilo, baada ya kufanya utafiti kujua hasa wazee hao wana uhitaji wa aina gani.
Baada ya kufanya hapa, wiki hii wanaendelea - na hapa ni kwa ajili ya wahanga wa kiafya, yaani wale waliojifungua kwa matatizo kwenye hospitali ya CCRBT. Japo hawana pesa nyingi
Mwisho wa yote Bwana Mpella anaiasa jamii ijifunze kukumbuka wasiojiweza, "sisi sote ni vijana, ila mwisho wa yote nasi tutafikia umri huo - hivyo ni vema kujifunza ni mambo gani unaweza kukutana nayo."
Kuna kinamama wana matatizo ya fistula, wakatengwa na jamii na kuna watoto wana matatizo ya kuwa na vichwa vikubwa - hawa wote wamekuwa wakipata misaada kwa namna mbalimbali, lakini ukiangalia wazee - hili ni kundi la watu waliosahaulika, ndio maana Praise Power Radio - Faraja ya Watu na kanisa la Mlima wa Moto tukafanya jambo hilo, baada ya kufanya utafiti kujua hasa wazee hao wana uhitaji wa aina gani.
Baada ya kufanya hapa, wiki hii wanaendelea - na hapa ni kwa ajili ya wahanga wa kiafya, yaani wale waliojifungua kwa matatizo kwenye hospitali ya CCRBT. Japo hawana pesa nyingi
Mwisho wa yote Bwana Mpella anaiasa jamii ijifunze kukumbuka wasiojiweza, "sisi sote ni vijana, ila mwisho wa yote nasi tutafikia umri huo - hivyo ni vema kujifunza ni mambo gani unaweza kukutana nayo."
Comments
Post a Comment