BABA, MAMA NA MKE WA MFANYA BIASHARA WANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KIJANA HUYO KUKIMBILIA KANISA LA MLIMA WA MOTO
Kibuyu kidogo chenye nembo ya twiga
Akionyesha moja ya dawa hizo
Maombezi
Ni ushuhuda uliosisimua mioyo ya maelfu ya watu
waliohudhuria katika ibada jumapili hii. Kijana huyo mfanya biashara wa bidhaa
ya duka katika soko la Tandale Uzuri, baada ya kuona biashara yake inalegalega,
alipata ushauri wa kuwaona wataalam, ndipo alipomtafuta mganga wa kienyeji na
kukabidhiwa dawa mbalimbali.
Hakika haijawahi kutokea, katika madhabau ya Mlima
wa moto chini ya usimamizi wa Mchungaji Kiongozi Dk. Getrude Rwakatare na
watumishi wengine, lilifunguliwa begi kubwa lililokuwa na dawa za aina
mbalimbali zikiwepo zile za kuwafanya wateja wasione fremu za watu wengine
isipokuwa duka lake. Dawanyingine ni kibuyu chenye picha ya twiga kikiashiria
kwamba yeye atakuwa juu kuliko wafanya biashara wenzake na nyingine ya yenye
noti zinazoashiria kuvuta pesa kutoka
kwa wafanya biashara wenzake na wateja.
Kilichomfanya kijana huyo kukimbilia kanisani usiku
wa manane na kuruhusiwa kulala kanisani, ni pale alipopigiwa simu baada ya
kuondoka kwamba, awe tayari kutoa damu; na damu hiyo si damu ya mbuzi wala ng’ombe
bali damu ya binadamu ambao ni Baba, Mama, ndugu wa karibu na hatimaye mke
wake.
Kijana huyo aliyekuwa amezilipia dawa hizo malaki ya
pesa, alichanganikiwa ghafla na hali yake kubadilika, ndipo alipokimbilia
kanisani; na baada ya kuona mlango wa kanisa mida ya saa saba usiku, ndipo hali
yake iliporejea kuwa nzuri. Kijana huyo amefanyiwa maombi na sasa Anamshukuru
Mungu wa Mlima wa Moto kwa Kumfungua.
Comments
Post a Comment